Tuesday 30 May 2017

Polisi Sumbawanga ashikiliwa kwa kuua

Na Gurian  Adolf
Sumbawanga

JESHI la  polisi mkoani Rukwa linamshikilia askali polisi wake anayefahamika kwa jina la  Prudence Michael  kwa kosa la  kuendesha gari kwa uzembe na kumgonga mtoto Brighton Apollo(3) na kumsababishia kifo chake.

Kamanda wa polisi mkoa  wa Rukwa George Kyando alisema kuwa kitendo cha kumgonga mtoto huyo  kilisababishwa na uzembe wa dereva barabarani kwani anapaswa kuwa makini  kwakua barabara  inatumika na watu wazima, watoto na viumbe wengine.

Tukio hilo lilitokea jana  Mei 29 majira ya saa  11 za jioni wakati polisi huyo  akiwa anaendesha gari la  jeshi  hilo maeneo ya jangwani ambapo alimgonga mtoto huyo.

Alisema kuwa kufuatia tukio hilo polisi inamshikilia askari huyo  na anatarajiwa kufikishwa mahakamani kutokana na tukio hilo.

Aidha Kamanda Kyando alitoa wito kwa madereva kuwa makini  pindi  wawapo barabarani wanaendesha vyombo vya moto ili kuepuka ajali za kugonga  ama kusababisha uharibifu wa Mali kwa kugonga  au hata wao wenyewe usalama  wao kwakua ajali inapotokea inasababisha madhara makubwa.

Hata hivyo alitoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kufuatia msiba huo na kuendelea kusisitiza umakini kwa watumia Barabara kwa madereva pamoja na watembea kwa miguu kwani yeye binafsi na  jeshi hilo wanasikitishwa kutokana na ajali hizo.
 
Mwisho

1 comment: