Wednesday 10 June 2015

Maelfu washindwa kujiandikisha baada ya muda kuisha

Image result for picha za watu wakijiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kuraNa Gurian  Adolf
Sumbawanga

ZAIDI ya watu 8877 wa kata za Kilangawane na Kipeta wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa hawatapata fursa ya kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao kutokana na kutoandikishwa katika daftari la kudumu la wapigakura baada ya muda kumalizika bila wao kupata nafasi hiyo.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na mbunge wa jimbo la Kwella Ignas  Malocha, afisa mtemdaji wa kata ya Kipeta Joseph  Ninde alisema kuwa mpaka siku zilizotolewa na tume ya uchaguzi zinamalizika  jumla ya watu 3,776 ndiyo walioandikishwa ambapo matarajio ilikuwa ni kuandikisha watu 8,651.

Alisema kuwa kushindikina kuandishwa kwa idadi kubwa hiyo ya watu ni kutokana na tangu  june 21 zoezi hilo lilipoanzishwa katika kata hivyo mashine zilizokuwa zikitumika zilikuwa mbovu na na hivyo kusababisha changamoto hiyo.

Naye kaimu afisa mtendaji wa kata ya Kilangawane Eliasi Kamkwamba alisema katika kata hiyo idadi ya watu ambapo walikuwa na sifa ya kuandikishwa katika daftari hilo walikuwa 7,846 lakini ni watu 4,002 ndiyo waliyoandikishwa na hivyo wengi wao pia huenda wakakosa haki yao hiyo ya msingi.

Kwaupande wake mbunge wa jimbo la Kwella Ignas Malocha ameiomba tume ya taifa ya uchaguzi NEC kuhakikisha inarudi tena ili iendelee kuandikisha watu waliokosa fursa katika zoezi la kwanza kwani huko ndiyo kutakuwa kuwatendea wananchi hao haki yao ya kikatiba.

Alisema kuwa bila kuogopa gharama tume ya uchaguzi inapaswa kurudisha mashine za BVR katika kata ambazo watu hawakujiandikisha na wajiandikishe kwani daima wanapaswa kutambua kuwa Demokrasia inagharama zake na kitendo cha kukwepa gharama ni kuifinyanga katiba pamoja na Demokrasia.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment