Thursday 19 December 2013

VIBAKA WATEMBEZA KIPIGO KATIKA BAA MBALIMBALI SUMBAWANGA



BAADHI ya wakazi wa mji wa Sumbawanga mkoani Rukwa wamelelamikia kuwepo kwa  kundi la vibaka wanaoendesha vitendo vya uvamizi katika maeneo tofauti ya kuuzia vilevi na kisha kuwatembezea kipigo watu wanaowakuta katika maeneo hayo na  kuwapora vitu mbalimbali ikiwemo fedha taslimu.

Kikundi hicho kimekuwa kikivamia katika baa zilizopo uchochoroni na kisha kuwalazimisha wateja wanao wakuta kutoa simu na fedha walizonazo na kisha kumvamia muhudumu na kuchukua fedha zote za mauzo na kuondoka nazo kuelekea kusikojulikana.

Peter  Joachim ni mmoja wa watu walivamiwa katika baa  ijulikanayo kwa jina la Lusaka Pub iliyopo mjini humo alisema kuwa wakiwa wanaendelea na burudan zao majira wa saa 5;15 za usiku lilitokea kundi la watu sita wakiwa na nondo na mapanga na kuingia ghafla ndani ya baa hiyo na kuwataka walale chini na kwa yeyote atakaye kataa kutii amri hiyo atauawa.
Alisema kutokana na silaha hizo walizokuwa nazo watu wote walilala chini na kisha vibaka hao waliwataka watoe fedha zote walizokuwa nazo pamoja na simu na kisha kuanza kuwakagua na waliporidhika kuwa hawanakitu waliondoka zao.
Katika tukio jingine lililotokea katika eneo la Wajanja Pub kundi la watu waliokuwa na mapanga, marungu na nondo walivamia katika baa hiyo ambapo walimkuta mtunza hazina wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Rukwa  na kisha kumpora fedha zaidi ya shilingi 200,000 na kuondoka nazo.
Mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina la Lingatsova alivamiwa akiwa mlangoni kwake na kundi la watu wasiojulikana  na kisha kumpiga nondo katika maeneo mbalimbali ya mwili wake na kisha kumpora fedha taslimu kiasi cha shilingi 250,000 pamoja na simu aina ya Sumsung Galaxy na kisha kuondoka nazo.
Baada ya kumpora  mtunza hazina huyo  vibaka hayo walivamia  katika nyumba ya mwanamke mmoja ili nako wafanye uporaji huo lakini mwanamke huyo aliwaona na kupiga kelele  ambapo vibaka hao walitimua mbio na kuelekea kusikojulikana.

No comments:

Post a Comment