Friday 20 December 2013

KING'AMUZI CHA TING CHAZINDULIWA RUKWA.



KAMPUNI ya AGAPE  televisheni  imezindua na kuanza kuuza kisimbusi  chake cha aina ya  TING mkoani Rukwa ili kutoa fursa kwa wakazi wa mkoa huo kuanza kutumia teknolojia ya digitali ambapo wataweza kuona channel nyingi tofauti na kutumia teknolojia ya Analojia  ambayo haitoi fursa ya kupata chaneli nyingi kama ilivyo kwenye Digitali.

Akizindua kisimbusi  hicho kwa niaba ya mkuu wa mkoa  huo ,makamu  mwenyekiti wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga  Emmanuel  Malisawa  alisema kuwa hii ni fursa kwa wakazi wa mkoa huo kuingia katika mfumo wa digital mapema zaidi kuliko kusubiri mpaka serikali itakapo zima mitambo ya Analojia ndipo waanze kutumia visimbusi vitakavyo wawezesha kupata matangazo ya televisheni.

Alisema kuwa  mabadiliko hayo ya kiteknolojia ni fursa nzuri kwa wakazi wa mkoa huo ambao ulikuwa haupati vyombo vya habari vingi katika mfumo wa analojia lakini kwa mfumo huu mpya wakazi wake watakuwa na uamuzi wa kuchagua kuangalia televisheni wanayotaka.

Naibu meya alisema kuwa kutokana na madiliko hayo wakazi wa Rukwa wanafursa ya kujua mambo mengi ikiwemo na masuala ya kibiashara ambapo kupitia ongezeko la vyombo vya habari wataweza pia kujua bei ya vitu mbalimbali ikiwemo soko la zao la mahindi ambalo imekuwa ni tatizo kwa wakulima waliopo mkoani humo.

Kwaupande wake mkurugenzi wa  Kampuni ya Agape  Televisheni  Vennon  Fernandos wanaomiliki kisimbusi cha TING  alisema kuwa wameamua kuja mkoani Rukwa kwa nia mbili kwanza ikiwa ni kutoa fursa kwa wakazi wa mkoa huo kuingia katika mfumo wa digitali mapema zaidi ambapo watapata nafasi ya kusikia na kujifunza mambo ya watu wengine sambamba na wao kutangaza yakwao.

Alisema kuwa sababu nyingine ni kuhubiri neno la mungu kupitia chaneli za kidini zinazopatika katika kisimbusi hicho ambapo kinaongeza wigo wa kusikia neno la Mungu hata ukiwa nyumbani kwako injili itakufikia hapo ulipo.

No comments:

Post a Comment