Saturday 21 December 2013

JELA MIAKA 60 KWA UNYANG'ANYI WA SILAHA.



WAKAZI wawili  wa kijiji cha Kakese  John Mwakalebene  (24)  na Kamili Lugoye  (30)  wametiwa  hatiani   na kuhukumiwa na makakama  ya wilaya ya  Mpanda mkoani Katavi   kutumikia  kifungo cha miaka 60 jela kwa pamoja  baada ya kupatikana na hatia  ya unyang’anyi wa kutumia silaha.


Hukumu hiyo ilitolewa  na Hakimu Mkazi Mfawidhi  wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda  baada ya mahakama kutokuwa na shaka na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na pande  mbili za mashitaka na utetezi ambapo kila mmoja atatumikia kifungo cha miaka 30 jela.



Washitakiwa hao  walidaiwa kutenda kosa hilo  la unyang’anyi hapo Julai  7 mwaka huu saa mbili  na nusu usiku kijijini hapo ambapo  walimshambulia kwa mapanga Tija Sailasi  na kisha kumpora fedha tasilimu  Tsh 430,000.



Katika tukio hilo pia walipola simu mbili zenye thamani ya shilingi laki moja vitenge  vya wax  bunda za sigara aina ya SM  na  vocha  na kufanya vitu thamani ya vitu na pesa  walivyopola  kuwa na jumla ya  Tsh  760,000


Akisoma hukumu  hiyo  Hakimu,  Chiganga  Ntengwa  baada ya kusikiliza mwenendo mzima  wa kesi mahakama  yake imewaona  washitakiwa  wamepatikana   na kosa  kwa mujibu  wa sheria  namba 287(A) ya sura ya 16 ya marekebisho ya mwaka 2009

Washitakiwa wakijitetea waliiomba mahakama hiyo iwapunguzie adhabu  kutokana na umri wao kuwa mdogo na wameoa hivi karibuni na wazazi wao wanawategemea lakini  baada ya maombi hayo, mwendesha mashitaka Mkaguzi msaidizi wa Polisi, Ally Mbwijo  alipinga vikali  na kuiomba  mahakama itoe adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hizo kwani vitendo hivyo vimeshamiri sana Mkoa wa Katavi.

No comments:

Post a Comment