Wednesday, 7 March 2018

waziri aagiza kuundwa tume kuchunguza miradi ya maji

Na Gurian Adolf
Nkasi
WAZIRI wa maji na umwagiliaji mhandisi Isack Kamwelwe ameagiza kuundwa  timu maalumu ambayo itakuwa na kazi ya kukagua miradi ya maji inayotekelezwa mkoani Rukwa kutokana na kuwa na mapangufu mengi ya kiufundi ambayo aliyabaini wakati akiwa anakua miradi hiyo.
Agizo hilo alilitoa jana katika Kata ya Kabwe wilayani Nkasi katika mkutano wa hadhara baada ya kubaini mfumo wa umeme wa jua unaotumika katika mashine ya kusukuma maji katika tenki kuwa hazina kiwango ambapo alidai kuwa haziwezi kudumu kwa muda mrefu.
Alisema kuwa yeye binafsi akiwa ni waziri mwenye dhamana hajaridhishwa na kasoro nyingi alizoziona baada ya kukagua mradi wa maji wa Kabwe ambao umejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 1.1 lakini ueonekana kuwa na changamoto hata kabla ya kuanza kutumika.
Waziri Kamwelwe alisema kuwa ameona mfumo huo wa umeme uliotengenezwa na kampuni ya A and O Consultant yenye makazi yake jinini Dar es salaam kuwa vifaa vilivyotumika havina ubora unaotakiwa hivyo ameagiza wizara yake iunde timu ya wataalamu watakao kagua miradi yote ya maji mkoani humo.
Alisema kuwa halmashauri ya wilaya ya Nkasi inamiradi ya maji nane yenye thamani ya shilingi bilioni 19 lakini miradi mingi inaonekana inahitilafu za kiufundi hivyo haina budi kukaguliwa ili kujiridhisha kwani serikali haipo tayari kuona fedha za walipa kodi zinachezewa hovyo.
‘’naagiza lazima iundwe timu ya wataalamu kutoka wizarani wafike kukagua miradi yote ya maji katika mkoa wa Rukwa,kwani imekuwa ikilalamikiwa sana, serikali ya awamu ya tano haitavumilia kuona fedha za walipa kodi zinatumiwa vibaya na watu wachache kwa manufaa yao’’ alisema.
Awali akimkaribisha waziri huyo afisa tawala wa wilaya ya Nkasi Festo Chonya alisema kuwa miradi ya maji inayotekelezwa wilayani humo imekuwa na changamoto nyingi ambapo inaonekana baadhi ya watekelezaji wamekuwa wakihujumu kwa makusudi.
Alisema kuwa miradi hiyo iliyotekelezwa imetumia fedha nyingi lakini kunahofu kuwa haitadumu kwa muda mrefu kutokana na vifaa vilivyo tumika kutokuwa imara kwani baadhi vimeanza kuharibika hata kabla ya miradi kuzinduliwa.
Naye mbunge wa jimbo la Nkasi Kusini Ally Kessy aliwashauri wananchi kuacha tabia ya kujisaidia ziwani kwani wamekuwa wakisababisha miripuko ya magonjwa kama kipindupindua mara kwamekua wakitumia maji hayo ya ziwani kwa kunywa bila kuchemsha.
Alisema kuwa ziwa hilo maji yake bado ni masafi kwani hayachafuliwa na kemikali mbalimbali changamoto iliyopo ni wananchi kujisaidia ziwani kutokana na kutochimba vyoo kitendo ambacho ni hatari kwani miradi ya maji inachukua maji hayo ya ziwa kwenye mabomba na kuwapelekea wananchi kwaajili ya matumizi yao.
Mwisho

No comments:

Post a Comment