Wednesday, 7 March 2018

wanafunzi wajeruhiwa na gari la jeshi

Na Israel Mwaisaka
Nkasi

WANAFUNZI wawili  wilayani Nkasi Mkoani Rukwa wamenusurika kifo baada  ya kugongwa na kujeruhiwa na gari la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)  katika  kijiji cha
Paramawe wilayani Nkasi  mkoani humo.

 Akizungumzia tukio hilo lililotokea jana majira ya saa 8;15  mchana
 katika kijiji cha Paramawe Kamanda wa Polisi mkoa
wa Rukwa George Kyando aliwataja majeruhi hao kuwa ni
Trivol Julius (12) ambaye ni mwanafunzi  wa darasa la nne Shule ya
Msingi Paramawe  na Isack Lusembo (17) ambaye ni Mwanafunzi wa
Kidato cha Nne katika Shule ya Sekondari Mtenga .

  Alisema kuwa chanzo cha ajili  hiyo ni mwendo kasi na uzembe wa
dereva  ambaye jina lake  limehifadhiwa.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo ambao hawakutaka majina yao yaandikwe gazetini walieleza kuwa Isack
ambaye ni mwanafunzi wa Kidoto cha Nne kabla ya ajili  hiyo alikuwa amembeba
Trivol kwenye baskeli  aliyokuwa akiendesha katika baraba ku itokayo
Tunduma mkoani Mbeya kwenda Mpanda mkoani Katavi katika eneo la kijiji cha
Paramawe.
Alisema kuwa wanafunzi hao wakiwa wanaendelea kuendesha baiskeri waliyopanda ghafla gari hilo la jeshi lilitokea nyuma yao likiwa na kasi kubwa ambapo liliwagonga na walianguka na kupoteza fahamu papo hapo.

Naye mkuu wa Wilaya ya Nkasi Said Mtanda ambaye jana usiku aliwatembea
majeruhi  hao ambao wamelazwa katika hospitali  Teule ya Wilaya  (DDH)
iliyopo mjini Namanyere  kwa matibabu alisema kuwa hali zao  ni mbaya
kwamba wanatarajiwa kuhamishiwa katika Hospitaliya rufaa  ya mkoa wa
Rukwa iliyopo mjini Sumbawanga kwaajili ya matibabu zaidi.

Mwisho

No comments:

Post a Comment