Na Walter Mguluchuma
Katavi
WATENDAJI wa jeshi la polisi mkoani Katavi
wametakiwa kufanya
kazi zao kwa kuzingatia
maadili na uzalendo ili
waendelee kuaminiwa na kujijengea
heshima kwa jamii.
Kamanda wa polisi mkoani humo Damas Nyanda aliyasema hayo jana katika
kantini ya Polisi wakati wa hafla ya makabidhiano ya bati
bandro 40 zilizotolewa na
wadau pamoja na askari polisi kwaajiri ya
ujenzi wa ukumbi wa kisasa utakao tumika kwaajili ya mikutano na sherehe.
Alisema kuwa ili polisi
aweze kujijengea heshima
kwa jamii ni
lazima wafanye kazi
kwa kuzingatia maadili na wawe wazalendo na hali itakayo wajengea heshima na imani.
Kamanda Nyanda alisema kuwa kutokana na polisi hao kutenda kazi kwa uweledi wadau hao wamewachangia michango
mbalimbali ambayo imefikia kiasi cha shilingi milioni 31,221,000.00 ambapo kati ya fedha hizo
Shilingi milioni 12,129,000
zimechangwa na askari
polisi na shilingi milioni 19,092,000 zimechangwa na wadau wengine wa maendeleo.
Aidha kamanda huyo wa polisi aliwashuru
wadau wote waliochangia na kuwaomba waendelee
na moyo huo na
usiwe kwa polisi
pekee bali wafanye hivyo na kwenye taasisi
nyingine pia ambazo zinahitaji misaada ya
michango ya maendeleo.
Naye mkuu wa wilaya ya Mpanda
Lilian Matinga alisema
kuwa mkoa wa
Katavi unao wadau
wengi wa maendeleo na wamekuwa
wakichangia kwenye maswala
mbalimbali ya maendeleo kwenye
jamii kama vile
elimu afya
na maji.
Kwa upande wake mbunge
wa Jimbo la
Mpanda mjini Sebastiani
Kapufi alisema yeye kama
Mbunge hataacha kuwazungumzia askari
polisi ndani
na nje ya bunge
juu ya changamoto
walizonazo askari hasa suala la nyumba za kuishi.
Alisema askari
polisi wanafanya kazi
kubwa ya
kulinda usalama wa raia
na mali zao na
jitihada hizo zinaonekana katika mkoa wa Katavi
kwani wameweza kupunguza matukio ya
uharifu na ujambazi yaliyokuwepo
miaka ya nyuma katika mkoa huo hali
ilyokuwa ikiwalazimisha baadhi ya wafanyabiashara kuhama
nyumba zao nyakati za
usiku kwa kuhofia
kuuawa.
Katika hafla hiyo msimamizi wa
mradi huo mratibu wa
polisi Kway Ngoroma
alisema kuwa fedha hizo
walizopata watahakikisha wanazitumia vizuri na kwa malengo yaliokusudiwa na
singinevyo.
Alisema mbali ya mradi
huo wa ujenzi wa
ukumbi wa mikutano pia kunasuala la ujenzi wa zahanati ya polisi ambao unaendelea ambayo
ikikamilika itasaidia
askari polisi kupatiwa matibabu na jamii
ya wakazi wa manispaa ya
Mpanda kwa ujumla.
Mwisho
No comments:
Post a Comment