Na Gurian Adolf
Sumbawanga
WATEJA wa bidhaa mkoani Rukwa wameonywa tabia ya kutodai risiti kwani wanaweza kujikuta wakifungwa jela miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi milioni 4.5
Akizungumza jana mjini Sumbawanga katika
maadhimisho ya wiki ya mlipa kodi meneja wa mamlaka ya mapato TRA mkoani
humo Fredrick Kanyilili alisema kuwa wateja hao wa bidhaa mbalimbali
wanapaswa kutii sheria ya mwaka 2015 kifungu cha 86 ambayo inatoa adhabu
hiyo. Sumbawanga
WATEJA wa bidhaa mkoani Rukwa wameonywa tabia ya kutodai risiti kwani wanaweza kujikuta wakifungwa jela miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi milioni 4.5
Naye meneja msaidizi mkaguzi wa TRA mkoani humo Amina
Shamdas
alisema kwa upande wa wafanyabiashara wao wameanya kuwa na mwitikio
mzuri katika matumizi ya mashine za EFDs ambapo mpaka sasa mkoa mzima
una wafanyabiashara 430 wanatumia mashine hizo.
Shamdas alisema kuwa upande wa vituo vya kuuzia mafuta mkoani humo wao wametii maelekezo ya kutumia mashine za EFDPs na mpaka sasa hakuna kituo ambacho kimekiuka agizo hilo.
No comments:
Post a Comment