Na Walter Mguluchuma
Katavi
WATU watatu wanaosadikiwa
kuwa ni majambazi walivamia machimbo ya
madini ya dhahabu ya Ifumile Kijiji cha
Isumamilomo Tarafa ya Nsimbo
Wilaya ya Mpanda na kumuua mchimbaji
mmoja kwa kumpiga
risasi tumboni kwa kutumia bunduki ya
kivita aina ya AK 47 nakisha kujeruhi wengine watatu na kupora dhahabu yenye uzito wa
zaidi ya Gramu 600,fedha tasilimu shilingi milioni 1.5 na mashine
mbili za kutafutia dhahabu.
Kamanda wa Jeshi la
Polisi wa Mkoa wa
Katavi Damas Nyanda
aliwaambia wandishi wa habari
kuwa tukio hilo lilitokea juzi
majira ya saa 2
usiku katika machimbo.
Alisema
siku hiyo ya tukio
majambazi hao ambao waliokuwa watatu
walifika katika machimbo ya
dhahabu ya Ifumile yaliko katika
Kijiji cha Isumamilomo
huku wakiwa wamejifunika
sura zao kininja na kuwashambulia
kwa risasi wachimbaji na
wanunuzi wa dhahabu kwenye
machimbo hayo .
Katika shambulio hilo
waliweza kuwajeruhi wachimbaji wanne katika
sehemu mbalimbali za mili yao huku
baadhi ya wachimbaji waliokuwa
kwenye eneo hilo
waliweza kusalimika baada
ya kuwa wamekimbilia kwenye
vichaka.
Kamanda Nyanda alimtaja aliyeuwa kwa kupigwa
risasi kuwa ni Sita Kalyalya (34)
Mkazi wa Bariadi Shiyanga
ambae alipingwa risasi ya
tumboni na mkononi
na aliyefariki dunia muda mfupi
baada ya kufikishwa katika Hospitali ya
Manispaa ya Mpanda wakati
akiwa anapatiwa matibabu.
Aliwataja pia waliojeruhiwa
kuwa ni Joseph Panya(34) ambaye amejeruhiwa kwenye bega la kushoto
na mguu wa kulia mwingine ni Mrisho
Rashid (21 ) aliyejeruhiwa mguuni
na mkono wake wa kulia
na Masunju Mgulu (28)
aliyejeruhiwa mguu na mkono wake
wa kushoto .
Kamanda Nyanda alisema
majambazi hao watatu hao baada
ya kuwajeruhi wachimbaji hao walipora fedha tasilimu
Tshs 1,500,000 Gramu
650 za madini ya dhahabu
na mashine mbili za
kutafutia madini na
kisha kutokomea kusiko julikana.
Mara baada ya tukio hilo
polisi walifika eneo hilo hata
hivyo waliweza kuokota risas
24 na
maganda saba ya
risasi zilizotumika za bunduki ya
kivita aina ya AK 47 iliyotumika kwenye
tukio hilo.
Alisema Jeshi la polisi
Mkoa wa Katavi
bado linaendelea kuwasaka
majambazi hao na alitoa
wito kwa wananchi kutoa
ushirikiano kwa jeshi hilo
kwa kuwapatia taarifa
zitakazowawezesha kuwatia nguvuni
watuhumiwa watukio hilo .
Kaimu Mganga Mkuu
wa Hospitali ya Manispaa ya
Mpanda Dr
Jaffari
Masanja
alisema marehemu Kalyalya alifariki muda mfupi
baada ya kuwa
ametolewa kwenye chumba cha
upasuaji ambako alikuwa
akipatiwa matibabu ya kuunganishiwa utumbo
wake mkubwa ambao
ulikuwa umekatika kutokana
na kupigwa risasi
tumboni .
Alisema majeruhi Panya na
Rashid wao ambao walikuwa
wamelazwa katika wodi
namba moja wamepewa rufaa na
wamesafirishwa kwenda katika
hospitali ya Rufaa ya Muhimbili
kwa ajiri ya matibabu
zaidi baada ya hali zao kuwa mbaya
ambapo majeruhi Masunju Mgelu
yeye amebaki kwenye
hospitali hiyo huku
hali yake ikiwa inaendelea
vizuri.
Mwisho
No comments:
Post a Comment