Israel Mwaisaka
Nkasi
MKUU wa mkoa Rukwa Zelote steven amewaagiza Waajiri wote
mkoani Rukwa wahakikishe kuwa mabaraza
ya Wafanyakazi yanafanyika kwa mujibu wa
utaratibu uliowekwa ili waweze kupata nafasi ya kujadili mambo yao kwa kina.
Agizo hilo amelitoa jana kwenye sherehe za Mei mosi ambazo kimkoa
ziliadhimishwa wilayani Nkasi ambapo alidai kuwa mabaraza ya Wafanyakazi ni
muhimu yakafanyika mahali pa kazi kwa uhuru mkubwa na ni jukumu la waajiri
kuona mabaraza hayo yanafanyika na kwa kufuata taratibu zilizowekwa.
Mkuu wa mkoa wa Rukwa Zelote Steven
“ufike wakati Waajiri kubadili mawazo juu ya vyama vya
Wafanyakazi badala yake wanatakiwa kushirikiana na mabaraza hayo ya wafanyakazi
katika kutafuta suluhisho la matatizo kwa wafanyakazi itakayoweza kuleta
ufanisi mkubwa mahali pa kazi”alisema zelote
Sambamba na hilo ameziagiza halmashauri zote mkoani Rukwa
kuhakikisha kuwa wanayatumia mapato ya ndani katika kujenga nyumba za watumishi
wao ili kuweza kupunguza tatizo la uhaba wa nyumba kwa watumishi lililopo kwa
sasa.
Alisema moja ya mambo yanayochangia ufanisi mkubwa kwa
watumishi ni kuishi kwenye nyumba bora ambazo zitamfanya kuwa huru na kuweza
kutekeleza majukumu yao kwa uhuru mkubwa.
Awali ofisa kazi wa mkoa Niseteli Buleti alidai kuwa ofisi
yake ndiyo sehemu halisi ya kushughulikia matatizo ya wafanyakazi lakini
changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni ya wafanyakazi wengi kushindwa kufika
kwenye mashauri pale yanaposikilizwa na kupoteza haki zao za kimsingi.
Hivyo aliwataka wafanyakazi kutokuwa waoga katika kutetea
haki zao za msingi na kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa Wafanyakazi kufika kwenye mashauri pale yanapokuwa
yamepelekwa katika ofisi yake ili kuweza kupata haki wanazozistahili.
Sherehe hizo za Meimosi zilikwenda sambamba na kuwazawadia
zawadi wafanyakazi bora waliofanya kazi kwa kujituma katika mwaka huu wa 2017
Mwisho
No comments:
Post a Comment