Monday, 1 May 2017

Mkurugenzi, madiwani Kalambo watunishiana misuli

Peti Siyame
Sumbawanga

MADIWANI wa Halmshauri ya Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa wamemjia juu Mkurugenzi Mtendaji wa halmshauri hiyo , Simon Ngagani  wakimshinikiza asitishe mara moja  mkataba alioingia na Wakala , Amri Said Nyambele  kukusanya ushuru wa mahindi  kwamba ni batili.

Mwenyekiti wa Halmshauri hiyo , Daudi Sichone ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la madiwani wa halmashauri hiyo aliwahimiza  madiwani hao waeleze kuwa  wako tayari  halmashauri  hiyo  kuuvunja mkataba huo  kwamba  iko pia tayari  kulipa  wakala  fidia ya mkataba ambao  ni  kiasi cha Sh milioni 16.

Hayo yalijiri katika kikao cha baraza la madiwani  kilichoketi mwishoni mwa wiki  katika Mji wa Matai ambapo  kila upande  ulitupiana  lawama  ambapo Mkurugenzi Mtendaji , Ngagani alidai  madiwani  hao wanaupiga vita  mkataba huo  kwa maslahi yao binafsi huku madiwani kwa upande wao  wakimlalamikia  Ngagani  kuwa ana maslahi na mkataba huo .

Pamoja na vutanikuvute hiyo Ngagani alieleza kuwa  hayupo tayari kuuvunja mkataba huo  kwa kuwa ulifuata  taratibu zote za manunuzi  isitoshe  ukivunjwa madhara yake  ni makubwa kwa halmashauri hiyo.

“Mkataba huu unawalakini  una mapungufu makubwa  nasema hatuutambui  usitishe mara moja hauna maslahi kwa halmashauri  yetu “ alieleza diwani Legius   Boimanda.

Nae  diwani, Bernad  Maskini alisisitiza kuwa mkataba huo  ni batili  haukufuata utaratibu wa kufikishwa  mbele ya baraza la madiwani  ili waamue  nani apewe  uwakala wa kukusanya  ushuru wa mahindi  huku akisisitza kuwa wakala Nyambele  ana sifa hiyo kwa kuwa nae ni mfanyabiashara wa  nafaka .

 Diwani , Peter Simuyemba alishauri halmashauri  iingie mkataba na Serikali ya Vijiji  ya ukusanyaqji  wa  ushuru wa mahindi  ambapo watapanga malengo ya makusanyo hayo  badala  ya kuendelea kuwakumbatia mawakala  ambao wengi wao sio waaminifu .

“Vitu viwe  wazi ... msitupige pige chenga  mkataba huu  haukupitishwa na  sisi madiwani  uvunjwe mara moja  kwani hatuutambui “Diwani Edwin Msipi

Nae Mwenyekiti wa baraza hilo Sichone alilazimika  mara  kwa mara akiwataka  madiwani waeleze wazi kuwa  wako tayari  mktaba huo uvunjwe na  fidia  ya mkataba  kuilipwe kuliko kuendelea nao .

Mkurugenzi Mtendaji Ngagani akifafanua aliwaeleza madiwani hao kuwa  Kamati  ya Fedha na Mipango imekasimiwa  madaraka  ya kuteua  wakala ambapo Mkurugenzi Mtendaji  akisaini  unakuwa  ni mkataba halali  ambapo utaletwa mbele ya baraza la madiwani kama taarifa na si vinginevyo .

“Sababu za kuuvunja mktaba huu sijaziona ..ubadhilifu  haupo kwa kuwa wakala atakusanya ushuru kwa kutumia mashine za kielektroniki …taratibu zote za  manunuzi zilifuatwa  sijaelewa kwanini hamu mtaki wakala huyu  sasa mnataka  niamini  niliyoyasikia  kuwa baadhi yenu mnawataka  maofisa  watendaji wa vijiji  ili iwe rahisi  kupiga nao dili''.. alisema

Kwani  hamtaki  huyu wakala  wa mazao wakati ambapo  tuna mawakala  wengine  mnadani  kwanini nao hamjawakataa?  Lazima kuna jambo  sio bure” alisisitiza .

Akifafanua alisema kuwa wakala Nyambele  kwa kipindi cha mwezi mmoja tu ameweza  kukusanya  zaidi ya Sh  milioni 26  ikiwa ni ushuru wa mahindi tu  kwamba  mktaba wake ni  wa miezi mitatu  ambapo sasa  imebaki miezi miwili  ambapo ukivunjwa  mktaba  halmshauri italazimika kumlipa fidia  ya mktaba  ambayo ni aslimia 20 ya makusanyo  hivyo italazimika kumlipa  kiasi cha Sh milioni  16 .

“Katika kikao cha Kamati ya Fedha na Mipango  wajumbe nane  walimkubali  wakala huyo huku mmoja akipinga …tutaongea sana  kuuvunja mktaba  huu sio rahisi  isitoshe hadi sasa  sijaona sababu za maana  kinachoshangaza hata madiwani wa CCM waliukataa  hata  kwenye vizuizi  vya mazao  asiwekwe mtu  inanitia shaka sana  lakini kwanini hamuwazungumzii wakala wa minadani''

Mnataka  halmashauri  iwarudishe  maofisa watendaj wa vijiji  wakusanye  ushuru wa mazao ili madiwani wanufaike  kwakuwa  walishazoea wanapatapata kitu kidogo  iwapo  kama mtavunja  mkataba  huu  niwakikishie  halmshauri hii  itayumba kifedha na itakuwa hatarini kuvunjika “ alisisitiza .

Alifafanua kuwa Kamati ya Fedha na Mipango  ikiridhia  na Mkurugenzi Mtendaji akitia saini tayari ni mkataba halali .

 Kaimu Mwanasheria wa Halmshauri hiyo , Tutalemwa Mwenda  aliwatahadharisha madiwani  hao kuwa iwapo  kama mkataba  huo utavunjwa  basi wakala atalipwa  fidia  ya mktaba ambayo ni Sh milioni 16 za bure   kwa miezi miwili ambayo  hajafanyika  kazi .

 Ndipo Mwenyekiti Sichone alipoomba ushauri kutoka  kwa washiriki  baada ya kupata ufafanuzi wa kisheria kutoka kwa Kaimu Mwanasheria Mwenda.

Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kalambo , Hilaly Kazumba alishauri ili halmashaurihiyo  isipate hasara  imwache wakala huyo amalize  miezi miwili iiyobakia .

Nae Katibu wa CCM wa wilaya ya Kalambo , Robert Mwiga aliwataka madiwani  hao wasitoe maamuzi ambayo yataitia hasara halmshauri yao .

Akichangia Katibu Tawala wa Wilaya ya Kalambo , Frank Sichalwe alisema madiwani wakiendelea  kushikilia msimamo wao huo wataiingiza halmashauri hiyo katika mgogoro mkubwa.

Baada ya kutolewa kwa ushauri huo  ndipo Diwani Peter Simuyemba alipotaka  madiwani wapige kura  ili kuumaliza mzozo huo ambao  kura 15 hazikutaka  mkataba huo  uvunjwe  huku tano zikitaka uvunjwe .

Gazeti  hili lilizungumza na baadhi ya madiwani  na waalikwa  kando ya kikao hicho  kwa masharti  ya  kutoandikwa majina yao  gezetini ambapo madiwani walikiri kuwa waliketi  kikao cha siri  na kukubaliana  mkataba huo uvunjwe .

“Nashangaa sana  mwishoni  tumegawanyika  tuliketi  na kukubaliana kwa pamoja  mkataba huu ni batili uvunjwe  lakini tumeshindwa  tulikubaliana  kuwa  hata kama  wakala huyu afanye  vizuri au la hatumtaki “ alisema mmoja wao .

Baadhi ya waalikwa walidai kuwa madiwani hawamtaki  wakala huyo  kwa kuwa atawabana  kwa kuwa wengi wao ni wakulima wakubwa wa mahindi  kwamba wanataka wakala ambaye watamteua wao.
Mwisho

No comments:

Post a Comment