Saturday, 19 August 2017

Na walter Mguluchuma
Mlele
SERIKALI imeipandisha hadhi zahanati ya Inyonga iliyopo wilaya ya Mlele mkoani Katavi nakuwa hospitali ya wilaya baada ya kukidhi vigezo ili iwezekutoa huduma kwawananchi wa wilaya hiyo. 
Waziri wa  afya,Maendeleo  ya  Jamii,jinsia wazee  na  Watoto   Ummy  Mwalimu  ameipandisha   hadhi  Zahanati hiyo jana mara  baada ya   kuikagua  na  kuridhishwa   na  vigezo   vinavyo  takiwa   vya  kuipandisha   hadhi  Zahanati  hiyo kuwa  hospitali ya   Wilaya.
 Alisema  amefikia maamuzi y'a kuipandisha   hadhi   zahanati  hiyo  kuwa  Hospitali ya wilaya   kutokana  na   mamlaka   aliyonayo   kama   Waziri wa  Wizara  husika.
Alivitaja  baadhi ya  vigezo  vinavyofanya iwe  na  hadhi ya  hospitali ya   Wilaya  kuwa  ni  huduma  ya  upasuaji ,Chumba  cha kuhifadhi  maiti , maabara , huduma ya  maji,umeme wa  uhakika  na  huduma ya  damu.
  Alifafanua  kuwa   kama   zahanati  hiyo  inatowa   huduma  kama   hospitali  ya  wilaya kwanini  yeye kama   Waziri  mwenye  dhamana  ashindwe  kuipandisha   hadhi  Zahanati   hiyo na   ukiangalia pia   Wilaya  hiyo  haina  Hospitali.
 Mwalimu   alisema   rais  John  Magufuli  alisha  waagiza   Mawaziri  kuwa  na  uamuzi wa  kutoa  maamuzi  magumu  pale   panavyositahili  kama ambavyo  alivyofanya  yeye  kuipandisha   hadhi   Zahanati  hiyo.
Alitoa  ahadi ya kupeleka  wataalamu  wengine haraka wezekanavyo  wenye   hadhi ya   kufanya  kazi   kwenye   Hospitali  hiyo   haraka  iwezekanavyo   kabla  ya  mwezi wa  Septemba  hauja  kwisha .
  Waziri huyo  alikabidhi  kwa  niaba  ya  rais  magodoro  20,vitanda  20 shuka  50 na vitanda  vitano vya kisasa  vya kujifungulia  akina mama wajawazito kwa  kwaajiri ya  Hospitali  hiyo ya  Wilaya.
Nae   Mganga   Mkuu  wa  Halmashauri ya  Wilaya ya Mlele  Dkt Luccy  Kafumu   alieleza  kuwa  mchakato  wa  maombi wa  kuipandisha   hadhi   zahanati  hiyo  ulianza  toka  mwaka  2013  baada ya wao  kuona  inasitahili kuwa  Hospitali ya   Wilaya .
  Dkt  Kafumu  alieleza  kuwa  Zahanati  hiyo  kwa  muda  wote toka  mwaka  2013  imekuwa  itoa  huduma  kama  hospitali ya  Wilaya  kwa   kitendo  hicho   cha   kuipandisha   hadhi  kitasaidia  hata  Mapato ya kununua  dawa  kuongezeka  kwenye  bajeti ijayo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment