Gurian Adolf
Sumbawanga
BAADHI ya wakazi wa maeneo ya Jangwani barabara
mbili (two ways) mjini Sumbawanga wako katika hatari ya kukumbwa na
magonjwa ya mlipuko ikiwemo ni pamoja na kipindupindu kutokana na
kutokuwa na tabia ya kufanya usafi.
Katika
baadhi ya maeneo hayo hali ni mbaya kutokana na kuwa na uchafu mpaka
vichichoroni huku katika mitaro ya kupitishia maji hali ndo mbaya zaidi.
rukwakwanza.blogspot
ilipata nafasi ya kuzungumza na wakazi hao walidai kuwa baadhi ya watu
wamekuwa hawana tabia ya kufanya usafi katika maeneo wanayoishi
wakiamini kuwa kazi hiyo ni ya Halmashauri ya Manispaa.
Mmoja
wa wakazi hao aliyejitambulisha kwa jina la Joseph Katanga alisema
kuwa wao hawapaswi kusafisha mitaro kwani si Mali yao kwakua mitaro hiyo
ni eneo la Manispaa wao jukumu lao ni kusafisha katika maeneo ya nyumba
wanazoishi.
Alisema kuwa
Halmashauri ya manispaa inapaswa kuajiri watu ama kuingia mkataba na
makampuni ili yaweze kufanya usafi lakini si kuwaambia wananchi
wakafanye usafi katika mitaro.
"Mitaro
ni Mali ya Manispaa hivyo basi mkurugenzi kupitia fedha anazopata
anapaswa kuajiri watu ama kuingia mkataba na makampuni ili yasafishe
lakini si kutuambia wakazi wa maeneo haya tufanye usafi".. Alisema.
Alisema
kuwa wao hawachafui mitaro hiyo ila ni baadhi ya watu wanaopita ndio
wanaotupa taka na nyasi zinaota na kwakua Manispaa haifanyi usafi ndiyo
maana hali inakua mbaya.
Naye
Maria Samaka alisema kuwa wapo watu ambao hua wanazoa takataka katika
mitaro hiyo lakini kwakua mji ni mkubwa wasipopita kwa siku mbili na
baadhi ya watu si wastaarabu wanatupa taka ndiyo maana inachafuka
nataka.
Alitoa wito kwa
wakazi wa mji huo kubadirika ki fikra na kupenda tabia ya usafi ili
mji wa Sumbawanga uwe msafi daima na wao waweze kuandoka katika hatari
ya kukumbwa na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment