Sumbawanga

Akizungumza na rukwakwanza. Blogspot.com meneja wa vipimo mkoani Rukwa na Katavi Abinery Nzanga alisema kuwa ni lazima wafanyabiashara wote katika mikoa hiyo kuhakikisha wanatumia mizani na kueleza kuwa baadhi kuzingatia uzito na si ukubwa wa magunia ambapo alitolea mfano kwa magunia Mkaa kg 30, mihogo kg 60, mchele 100 maharage 100, mahindi kg 100mpunga kg 75 na ngano kg 90.
Alisema kutokana na wafanyabiashara kutokuwa na utamaduni wa kutumia mizani umekuwa ukisababisha kutokuwa na usawa wakati biashara inapofanyika kwani mara nyingi wakulima wamekuwa wakidhurumika kwani wafanyabiashara wamekuwa wakipima bidhaa kwa wakulima kwa kutumia madebe lakini wao wanakwenda kuuza kwa kutumia mizani.
Nzunga alisema kuwa ili kutenda haki kwa makundi yote ni lazima kipimo cha mizani ambacho ndicho kinatambuliwa kisheria ndicho kinapaswa kutumika tofauti na hivyo ni ukiukwaji wa sheria na wao hawatakubali kuona kundi moja likidhurumika.
Naye Juma Chacha afisa vipimo wa wakara hiyo amesema kuwa hivi sasa wataendesha operesheni ili kuwakamata wafanyabiashara wanaokiuka sheria hiyo ili kukomesha biashara ambayo imekuwa ikifanyika bila kufuata sheria.
Kwaupande wao wafanyabiashara wa soko la Mandera mjini Sumbawanga walisema kuwa wao hawana tatizo na matumizi ya mizani kwani wakulima ndiyo wamekuwa wakigoma kutumia mizani kwakuwa hawajui kuisoma.
Walisema kuwa wakotayari kufuata matakwa ya sheria kwakuwa ndivyo inavyoelekeza ili kuepuka mkono wa shelia kwakuwa nao wanachotaka haki itendeke pindi wanapo fanya biashara zao na kusiwepo wa kupata hasara.
mwisho
No comments:
Post a Comment