Tuesday, 2 June 2015

WATANGAZA NIA YA URAIS WASICHAFUANE

Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mbunge wa Katavi).
Hakika Mungu ni mwema sana. Ametuwezesha leo kuwa na nguvu ya kutafakari hatima ya nchi yetu ambayo inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 hapo Oktoba.Mwishoni mwa wiki iliyopita tulishuhudia makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakijitokeza kuwania urais kupitia chama hicho na tayari wameanza kuchuana kutangaza nia yao baada ya vikao vya Kamati Kuu Taifa (CC) na Halmashauri Kuu Taifa (NEC) kumalizika hivi karibuni mjini Dodoma na kutoa baraka zote kuanza rasmi kwa mchakato huo.
Orodha ndefu ya makada walioonesha nia ya kutangaza kuwania ndani ya chama hicho ni Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa (Mbunge wa Monduli) aliyetangaza nia Arusha, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika,…
Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mbunge wa Katavi).
Hakika Mungu ni mwema sana. Ametuwezesha leo kuwa na nguvu ya kutafakari hatima ya nchi yetu ambayo inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 hapo Oktoba.Mwishoni mwa wiki iliyopita tulishuhudia makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakijitokeza kuwania urais kupitia chama hicho na tayari wameanza kuchuana kutangaza nia yao baada ya vikao vya Kamati Kuu Taifa (CC) na Halmashauri Kuu Taifa (NEC) kumalizika hivi karibuni mjini Dodoma na kutoa baraka zote kuanza rasmi kwa mchakato huo.
Orodha ndefu ya makada walioonesha nia ya kutangaza kuwania ndani ya chama hicho ni Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa (Mbunge wa Monduli) aliyetangaza nia Arusha, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Masatu Wassira (Mbunge wa Bunda) aliyetangazia nia yake Mwanza na Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Lameck Mchemba (Mbunge wa Ilamba Magharibi) aliyetangaza nia hiyo Dodoma na ambaye hivi karibuni alitangaza kujiuzulu nafasi yake ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Taifa ili aingie katika kinyang’anyiro hicho.
Wengine waliotangaza nia ni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli (Mbunge wa Chato), Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, Waziri Mkuu wa sasa, Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mbunge wa Katavi), Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu (Mbunge wa Singida Magharibi), Waziri wa Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi, Dk. Taitus Kamani (Mbunge Busega) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (Mbunge wa Mtama) aliyetarajiwa kutangaza nia jana jimboni kwake.
Wapo pia Waziri Asiye na Wizara Maalumu, Profesa Mark Mwandosya (Mbunge wa Rungwe Mashariki), Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba (Mbunge wa Bumbuli), Mbunge wa Jimbo la Sengerema, William Ngeleja na Mbunge wa Jimbo la Nzega, Dk. Khamis Kigwangalla.
Makada wengine ni pamoja na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Uchukuzi, Samwel Sitta (Mbunge wa Urambo Mashariki), Balozi Bi Amina Salum Ali (Zanzibar) na Mtoto wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyererer,  Makongoro Nyerere (sasa ni Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki). Hata hivyo, orodha hii inaweza kuongezeka kwa sababu wengine walikuwa wakisubiri kipyenga kipulizwe.
Kwa upande wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wao bado mchakato wao haujaanza kwa sababu watachuana baada ya kila chama kati ya vyama vya Chadema, Cuf, NCCR Mageuzi na NLD kutoa wagombea wao.
Ninachowaomba watangaza nia ni kwamba wasitumie mwanya huo wa kujitangaza kuchafua wenzao na badala yake wajenge hoja bila kupitiliza kwa sababu kampeni rasmi zinazosimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi bado hazijaanza.
Kila mtangaza nia anatakiwa ajipange kuja kuwaeleza Watanzania jinsi ya kuboresha maisha duni ya wananchi kwani walio wengi ni magumu.
Watangaza nia wajipange kueleza jinsi ya kuondoa mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali nchini ambao uko  juu, wajipange kueleza wataisaidiaje jamii? Niwaase watangaza nia hasa kutoka chama tawala CCM kwamba kila neno watakalokuwa wanalitamka litakuwa linapimwa na wananchi.
Kwa hiyo basi, watangaza nia watakaotumia majukwaa kuwachafua wenzao, moja kwa moja watakuwa wamekwenda ‘nje ya reli’ kwa sababu sasa hivi wananchi wanataka kiongozi ambaye ataeleza jinsi ya kuwakwamuwa kiuchumi, kimatibabu na kielimu.
Ni jambo la msingi sasa kwa wana CCM kupima wagombea wao na wasijazane tu kwenye mikutano ya kutangaza nia na kushangilia kishabiki bila kupima neno kwa neno.
Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

No comments:

Post a Comment