Sumbawanga
WAKURUGENZI wa halmashauri ya wilayani ya Sumbawanga na Manispaa mkoani Rukwa wameingia matatani kwa kitendo cha kuhamisha fedha za malipo ya wakandarasi na kuzipeleka kutengeneza madawati.
Akizungumza katika kikao cha Bodi ya barabara yamkoa huo mwenyekiti wa wakandarasi Anyosisye Kiluswa alisema kuwa fedha hizo kiasi cha shilingi milioni 250 wamekuwa wakizidai kwa muda mrefu pasipo mafanikio.
Alisema kuwa wakandarasi wa ndani wanadai fedha hizo tangu mwaka 2016 baada ya kukamilisha miradi ya maji,barabara, na ujenzi wa vyumba vya madarasa ambazo hawajalipwa kwa muda mrefu.
Kiluswa alisema kuwa fedha hizo zilikuwa ni za matazamio baada ya kukamilika kwa mradi ambazo zinapaswa kulipwa ndani ya kipindi cha miezi mitatu mpaka sita tangu kukamilika kwa mradi lakini ni zaidi ya mwaka na nusu hawajalipwa.
"wakandarasi walikwisha kamilisha miradi na wakakabidhi na ikapokelewa lakini mpaka sasa hatujalipwa madeni yetu kituambacho sio sahihi kwani halmashauri pamoja na Tarula wanatuweka katika wakati mgumu,kwani tumeelemewa na madeni" alisema
Alisema walipo kuwa wanatekeleza miradi hiyo fedha hizo zilikuwepo lakini watendaji wa halmashauri walibadili matumizi na kuzielekeza kwenye kutengenezea madawati kitendo kilicho sababisha wasilipwe mpaka sasa.
Mwenyekiti huyo wa wakandarasi alisema kuwa hivi sasa baadhi ya wakandarasi wanakabiliwa na madeni kwani baadhi yao walikopa fedha katika mabenki,huenda mali walizo weka dhamana zikapigwa bei na hivyo kujikuta halmashauri zimewasababishia umasikini wa kutupa.
"tunaiomba wizara ya ujenzi na miundo mbinu iingilie kati suala hili,ili tulipwe kwani imekuwa ni muda mrefu inasabaabisha tukwame katika shughuli zetu na hivyo kuishi kwa shida na kutoaminika tena kwani baadhi ya wanaotudai wanatuona kama matapeli hali inayotuvunjia heshma" alisema
Hata hivyo gazeti hili lilipo mtafuta mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Hamid Njovu ili kupata ufafanuzi wa madai hayo alisema kuwa halmashauri yake haidaiwi na mkandarasi yoyote kwani mpaka Tarula inaanzishwa halmashauri hiyo ilikuwa na fedha kiasi cha shilingi milioni 360 na angeweza kulipa.
Naye mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga John Msemakweli alisema kuwa baada ya kuanzishwa TARULA waliikabidhi kazi zote pamoja na madeni ya wakandarasi ndio wanapaswa kuyalipa.
Akizungumzia malalamiko hayo katika kikao cha bodi ya barabara ya mkoa katibu tawala mkoa wa Rukwa Bernard Makali alisema kuwa ataziandikia barua halmashauri hizo na TARULA wahakikishe wanalipa madeni hayo haraka iwezekanavyo kwani yamekuwa ni ya muda marefu.
Mwisho
No comments:
Post a Comment