Wednesday, 23 August 2017

Watanzania wapya waonywa

Na  Walter Mguluchuma
Katavi.
SERIKALI  imewaonya Watanzania wapya waliokuwa  raia wa  nchi  ya Burundi iwapo watabainika kujihusisha na uhalifu wa aina yoyote ile ikiwemo  kufanya mazoezi ya kivita,ujangili,ubaguzi wa kikabila na dini  haitasita  kuwafutia uraia wao na kuwarejesha Katika nchi walizotoka. 
Onyo hilo  limetolewa jana  na Waziri  wa Mambo ya ndani ya nchi , Mwigulu Nchemba  wakati akihutubia mkutano wa hadhara watanzania hao wapya wanaoishi katika makazi ya Katumba.
“ Wapo baadhi yenu ambao mmeshakubaliwa  na kupewa  uraia  wa nchi hii  zipo taarifa kuwa mnajihusisha na uhalifu  ikiwemo  ujingili katika hifadhi zetu pia mna ubaguzi wa  kikabila  ambapo mnawahamasisha wenzenu  wasinunue bidhaa kwenye maduka ya wafanya biashara wazawa wa nchi hui...  hii hatuwezi kukubali"...alisema
Waziri huyo aliongeza"wenyewe kwa wenyewe mnabaguana kwamba wengine mnatoka milimani na wengine chini ya milima  mkidharauliana  kuwa upande mmoja ni bora kuliko mwingine  huu si utamaduni wetu watanzania “... alisema
Aliwataka  wawe raia  wema na wazalendo huku akisisitiza kuwa Serikali imefanya kazi kubwa ya kuwapatia uraia ambapo mpaka sasa  kuna vyeti vya uraia vipatavyo 7,551 ambavyo havijachukuliwa licha ya wakimbizi walioomba kukubaliwa  kuwa watanzania wapya.
Alisema  Serikali   haiwezi  kuondoo   utaratibu wa  watu kuingia  kwenye   Makazi  hayo  bila  mtu kuwa  na kibali   mpaka  hapo itakapokuwa  imejiridhisha kuwa watu wanao ishi  kwenye  maeneo  hayo watakuwa wameacha vitendo vya uharifu.
Alifafanua  kuwa  yeye   kama  Waziri wa  Mambo ya  ndani ya  nchi  hata  kubali  kuondoa  vizuizi  vya    barabarani  kwenye   makazi   hayo wakati  mpaka  sasa kuna watu wanaotoka  kwenye   Makazi hayo wanaendelea kukamatwa  katika  matukio ya  ujangili na uharifu wa aina mbalimbali.
Aidha Serikali imekataa kuwapatia uraia wapatao 3,100 wakimbizi kutoka nchi jirani ya Burundi  wanao  ishi   katika  makazi  ya Katumba    na   Mishamo  Mkoani   Katavi   ambapo wakimbizi 900 wamekataliwa ni wakazi makazi ya  Katumba Wilayani   Mpanda  huku katika kambi ya Mishamo wilayani Tanganyika  ni wakimbizi 1,300  ambao wamekataliwa kutokana na sababu  mbalimbali
Kwa upande wake Mkuu wa  mkoa wa Katavi , Raphael Muhuga aliwataka wakimbizi wanaoishi katika kambi hiyo  ya Katumba ambao wanataka kurejea Burundi wawe huru  kwani milango  iko wazi la muhimu wazingatie na kufuata taratibu.
Aliwataka raia   hao wapya waendelee kutunza   mazingira  kama  ambavyo walivyokuwa wakiyatunza  kama  kabla ya kuwa  raia wa  Nchi hii.

Mwisho

No comments:

Post a Comment