Sunday, 20 August 2017

Madaktari bingwa wadaiwa kuwaacha solemba wagonjwa

Na Walter Mguluchuma
Katavi
Baadhi ya wananchi kutoka maeneo  mbalimbali ya mkoa  wa  Katavi wamelalamikia  kitendo kilichofanywa na  Madaktari bingwa cha kusitisha ghafla na bila taarifa huduma ya upimaji na utoaji wa  matibabu ya  magonjwa yasiyo ambukiza nakisha kuondoka nakuwaacha bila kuwahudumia. 
 Madaktari hao wa  magonjwa  mbalimbali  yasiyo  ambukiza wa kutoka tasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete na hospital ya Oceanroad walikuwa wakitoa huduma katika uwanja wa Polisi uliko  Manispaa ya Mpanda mkoani humo. 
Huduma za upimaji  wana utoaji wa matibabu ya  magonjwa  yasiyoambukizwa ulizinduliwa  juma  tano  ya  wiki  iliyopita  na  waziri wa  afya Maendeleo  ya  Jamii Jinsia Wazee na  watoto  Ummy  Mwalimu.
Madakitari  hao walikuwa  wameletwa  Mkoani Katavi  kwa  ajiri ya  kutoa  huduma  hizo na Mbunge wa  Viti  Maalumu mkoani humo Anna  Lupembe  ambae  alipita  katika  Wilaya  zote  tatu  za mkoa huo na  kuwatangazia  wananchi  na  kuwahakikishia  kuwa huduma  za madaktari  hao  zitakuwepo  hadi  siku ya ijumaa  lakini  zilisitishwa  siku moja kabla yaani  Alhamisi  na  kuwasababishia wananchi hasa  za  gharama  kwa  wananchi waliokuwa wametoka  vijijini.
Mkazi wa  Kijiji  cha  Karema  Said  Juma  alisema  yeye  ni  mmoja  wa   wakazi  wa  Tarafa ya   Karema  aliyesafiri  umbali  wa  kilometa  130 kwa  ajiri kufuata huduma zinazotolewa na madaktari  hao  lakini  alipofika  kwenye  eneo  waliokuwa wakitolea  huduma  alikuta   mabanda  yako  wazi   huku kukiwa  hakuna  daktari  bingwa  hata  moja nawagonjwa wamekaa.
Naye Abel  Kalifumu   Mkazi   wa  Tarafa ya  Inyonga  Wilayani  Mlele  alieleza  kuwa yeye  na  wenzake  walifika   Wilayani  Mpanda kwa   ajiri ya  kupatiwa  huduma  baada ya  Mbunge    Lupembe  kuwatangazia  kwenye  mkutano wa  hadhara  uliofanyika  siku ya  alhamisi   katika   viwanja  vya  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Mlele  kuwa  huduma  itakuwepo  mpaka  siku  ya  ijumaa na wakasafiri kesho yake alfajiri  lakini  walipofika mjini   Mpanda walikuta hakuna  huduma.
Jojina   Katumbo  mkazi wa  Tarafa  ya  Mpimbwe alieleza  kuwa  walitangaziwa  kwenye  mkutano wa  hadhara   uliofanyika  usevya  Wilayani  Mlele  kwenye  mkutano  huo  ambao  uliutubiwa   na    Waziri   wa afya Ummy  Mwalimu  kuwa   huduma  hiyo  itatolewa   mpaka  siku ya  ijumaa  lakini   haikuwa  hivyo.
Alisema kuwa kitendo hicho kimewasikitisha sana wananchi hao ambao walisema kuwa kama suala likikuwa ni malipo wangewaambia wauze hata mifugo na chochote ilimradi wapate huduma kwani wao kuwahudumia pale gharama ingekuwa nafuu kuliko kuwafuata Dar es Salam ambapo pia ni shida kuwapata. 
"Kwaweli kitendo walichotufanyia ni unyanyasaji kanakwamba sisi sio binadamu na hatunahaki ya kutibiwa na madaktari hao....basi acha tu tufe kwakua hatuthaminiki hatuna jinsi kwakua ni masikini"..alisema Moses Kaihero
"kinachotusikitisha nikutufanya tuone mpaka waziri wa afya alietuambia matibabu yapo mpaka siku ya ijumaa lakini wakayasitisha siku ya alhamisi kama nayeye alitudanganya tu,lakini labda kwakua ni mwanasiasa alikua anafanya siasa mpaka kwenye afya zetu"...alisema Richard Kayanda
Hata hivyo taarifa  za  kutoka  ndani ya  vyanzo  vya   habari  vinadai kuwa  kulikuwa  na  kutofautiana kwa  baadhi ya  makubaliano  baina  ya  madaktari  bingwa  na  mwenyeji  wao  ambaye ni mbunge Lupembe hali iliyopelekea hata mafuta ya gari aina ya basi walilokuwa wakilitumia madaktari hao lilitakiwa kuwekwa mafuta na mbunge huyo wakati wa kuwarudisha  Dar es  salaam lakini ilibidi yatolewe na  Ofisi  ya Mganga  Mkuu wa  Mkoa huo kutokana na tofauti iliyojitokeza. 
Mwisho

No comments:

Post a Comment