Thursday, 27 July 2017

Nkasi watumia mgambo kudhibiti mauaji

Na Israel Mwaisaka
 Nkasi .
SERIKALI  ya Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa imeziamuru  Serikali za Vijiji na Kata  wilayani humo kuwatumia  askari mgambo  maarufu askari wa akiba  kuimarisha  ulinzi na usalama katika maeneo yao  ili kukabiliana  na visa vya mauaji  vinavyofanywa na wananchi wanaojichukulia  sheria mikononi kila kukicha .
Agizo hilo lilitolewa  na Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Said Mtanda  ambaye pia kwa wadhifa wake ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi  na Usalama ya Wilaya kufuatia malalamiko  ya visa vya kihalifu  ikiwemo mauaji yanayofanywa kiholela  na wananchi  yaliyotolewa na baadhi ya madiwani  katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika  jana  mjini Namanyere wilayani hapa .
“Ni kweli hali ya ulinzi na usalama  katika baadhi ya vijiji wilayani hapa  sio ya kuridhisha kumekuwa  na visa vya unyanyasaji , ukatili , ubakaji na  mauaji yanayotokea  kila kukicha ambayo  nieleze wazi yanafanywa na  watu wa jamii  ya wafugaji ….
Sasa naa agiza Serikali za Vijiji na Kata zianze kuwatumia askari wa mgambo ambao tayari wamepatiwa mafunzo wasaidie  kuimarisha ulinzi  na usalama katika maeneo hayo  kwa kuwa  idadi ya askari polisi bado ni ndogo “ aliagiza DC .
Baadhi ya madiwani walieleza kuwa  katika kijiji cha Kasu  kilichpo wilayani  humo  kuna kikundi cha kihalifu  kinachojulikana  Fwaku Fwaku ambapo  juzi  mama mmoja alibakwa  lakini kwa aibu aliamua kunyamaza .
Mwisho

No comments:

Post a Comment