Thursday, 24 August 2017

Waomba madhehebu ya dini yafutwe


Na Walter Mguluchuma
Katavi
BAADHI ya watanzania wapya wanaoishi katika mkazi ya Katumba wilaya Mpanda katika mkoa wa Katavi wamemuomba  Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi iyafute baadhi ya madhebu ya dini yanachoche ubaguzi wa kidini Katika makazi yao.
Ombi  hilo waliliwasilisha jana kwa waziri Mwigulu Nchemba wakati alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara  katika makazi ya Katumba.
Mmoja wa wakazi hao Yusuf Shaabani alimweleza waziri  Nchemba  kuwa  ubaguzi wa kidini umekithiri kwenye makazi yao ambapo hata kuoana waumini wa madhehebu tofauti wanakataliwa.
Alisema kuwa wapo baadhi ya viongozi wa mathehebu wamekuwa wakihubiri chuki dhidi ya dhehebu jingine na hata kudiriki kuwakataza wafuasi wao wasioe muumini wa dhehebu jingine hata kama wawili hao wamependana.
Naye mkuu wa makazi ya  wakimbizi ya  Katumba  Athuman  Ingwe  alieleza  kuwa   Makazi  hayo ya  Katumba  yalianzishwa  mwaka 1973 huku   yakiwa  na  jumla ya  watu   78,201 na kwa  sasa  raia  wapya wakiwa ni  asilimia  98 na walibaki  bado ni  wakimbizi wa  nchi ya  Burundi .
“Zoezi la kuwahakiki wakimbizi wa nchi jirani wanaoishi katika kambi  hii ambao wanaomba uraia  limeanza tangu Juni mwaka huu ambapo hadi sasa wakimbizi wapatao 11, 329 ambao ni sawa na kaya 5,134 wamehakikiwa "alisema Ingwe.
Nae Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Richard Mbogo aliiomba Serikali  iliondoe eneo la ukubwa wa  ekari 145,000 ambalo wanaishi watanzania wapya  na wasio raia kutoka kwenye makazi ya wakimbizi Katumba  ili lote liwe makazi ya watu.
 Mbogo   aliomba   ufanyike  utaratibu wa  kuwapatia   elimu ya  uraia   Watanzania hao  wapya  ili  waweze  kutambua  sheria  za  nchi  na   katiba  ya  Tanzania ili waweze kuzifuata na kuziheshimu. 
Mwisho

No comments:

Post a Comment